Exodus 3:14-15

14 aMungu akamwambia Musa, “Mimi niko ambaye niko. Hivyo ndivyo utakavyowaambia Waisraeli: ‘Mimi niko amenituma kwenu.’ ”

15 bVilevile Mungu akamwambia Musa, “Waambie Waisraeli, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amenituma kwenu.’ Hili ndilo Jina langu milele, Jina ambalo mtanikumbuka kwalo kutoka kizazi hadi kizazi.

Copyright information for SwhKC